Skip to main content

Posts

Showing posts from March, 2015

Chicharito asema Real Madrid ni majanga tupu

 Mshambuliaji Javier Hernadez ” “Chicharito” amesema kuendelea kukaa benchi katika klabu ya Real Madrid kunamfanya akose furaha na kukosa kujiamini. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Mexico alijiunga na mabingwa hao wa Ulaya mwanzoni mwa msimu huu akitokea katika klabu ya Manchester United kwa mkataba wa mkopo wa mwaka mzima. Katika mkataba huo Real Madrid wanakipengele cha kumsajili moja kwa moja mshambuliaji huyo lakini hana uhakika kama ataendelea kubaki klabuni hapo. “Ninajitahidi kwa asilimia 100 kwenye mazoezi lakini kwenye mechi sichezi,hilo linaondoa kujiamini na ninakosa furaha” alisema Chicharito Tangu ajiunge na Real Madrid Chicharito amecheza mechi 13 za La Liga na kufanikiwa kufunga magoli matatu na kutoa pasi ya mwisho moja. Chicharito,26, alijiunga na Real Madrid mara baada ya kukosa namba katika kikosi cha Louis Van Gaal na pia kuwasili kwa mshabuliaji Radamel Falcao kulichangia kwa kiasi kikubwa. Mchezaji huyo ambaye mkataba wake katika klabu ya Manchester

New video: Shetta Ft. Kcee - Shikorobo - Official Music Video HD>>>Angalia hapa

Angalia hapa

Mapya ya Gwajima yazidi kuibuka Dar

Joseph Gwajima   MAPYA yamezidi kuibuka katika sakata la Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Joseph Gwajima, baada ya kuthibitika kwamba bastola iliyokamatwa katika harakati za kile kinachotajwa kutaka kumtorosha kutoka katika Hospitali ya TMJ, Dar es Salaam, ni mali yake. Aidha, mmoja wa wanafamilia, ameibuka na kuelezea kushangazwa na ujasiri alioupata Askofu Gwajima wa kumtukana Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Kardinali Polycarp Pengo, na kusema wanafamilia hawako pamoja naye katika hilo, huku wakimtaka amwombe msamaha Askofu Pengo. Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, alisema jana kuwa uchunguzi wa kina na wa kitaalam, sasa umethibitisha silaha hiyo inamilikiwa kihalali na Askofu Gwajima. “Kuhusu risasi 17 za short gun ni kwamba Askofu Gwajima anamiliki bunduki aina ya short gun yenye namba 102837 ambayo inatumia risasi za aina ya hizo zilizokamatwa,” alisema Kamanda Kova. Bastola hiyo ni moja ya vitu walivyokamatwa n

New video:Diamond Platnumz ft Khadija Kopa - Nasema Nawe HD>>Angalia hapa

Angalia hapa

Kafulila Aikana ACT- Tanzania...sina sababu ya kuhama chama changu

Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila, ambaye ni Katibu Mwenezi wa Chama cha NCCR-Mageuzi, amesema hana sababu yoyote ya kuhama chama chake na kujiunga na chama kipya cha siasa cha Alliance for Change and Transparency (ACT-Tanzania).   Kafulila alisema hayo jana alipokuwa akijibu swali kuhusu kusambaa kwa tetesi katika mitandao ya kijamii kwamba, anahamia chama hicho akiambatana na aliyekuwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe aliyehamia chama hicho hivi karibuni.   “Tetesi hizo zinatokana na tabia yangu ya kuwa na marafiki wengi katika chama hicho kipya, lakini nashangaa nina marafiki wengi CCM na hata Chadema, lakini hawasemi nahamia vyama hivyo ila ACT. Hizo ni tetesi tu sina sababu ya kuhama chama changu,” alisema.   Alisema Zitto alihama Chadema kutokana na mgogoro uliokuwepo baina yake na Chadema, hivyo alikuwa na sababu ila yeye akihama bila kuwa na sababu, itakuwa haina maana.   Alisema yeye bado ni Katibu Mwenezi wa NCCR-Mageuzi na anaendelea na kampeni z

Kafulila Aikana ACT- Tanzania...sina sababu ya kuhama chama changu

Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila, ambaye ni Katibu Mwenezi wa Chama cha NCCR-Mageuzi, amesema hana sababu yoyote ya kuhama chama chake na kujiunga na chama kipya cha siasa cha Alliance for Change and Transparency (ACT-Tanzania).   Kafulila alisema hayo jana alipokuwa akijibu swali kuhusu kusambaa kwa tetesi katika mitandao ya kijamii kwamba, anahamia chama hicho akiambatana na aliyekuwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe aliyehamia chama hicho hivi karibuni.   “Tetesi hizo zinatokana na tabia yangu ya kuwa na marafiki wengi katika chama hicho kipya, lakini nashangaa nina marafiki wengi CCM na hata Chadema, lakini hawasemi nahamia vyama hivyo ila ACT. Hizo ni tetesi tu sina sababu ya kuhama chama changu,” alisema.   Alisema Zitto alihama Chadema kutokana na mgogoro uliokuwepo baina yake na Chadema, hivyo alikuwa na sababu ila yeye akihama bila kuwa na sababu, itakuwa haina maana.   Alisema yeye bado ni Katibu Mwenezi wa NCCR-Mageuzi na anaendelea na kampeni z

Cleric Urges Nigerians To Accept Election Results As God's Will

As the nation awaits the results of the Presidential and National Assembly elections conducted yesterday and today, Nigerians have been urged to take the outcome of the results as the will of God. Pastor Olusola Adewumi of the Christ Apostolic Miracle Church, Ikole in Ekiti State made the call in his sermon to mark Palm Sunday in Ikole, Ekiti State. Adewumi attributed the successful conduct of violence-free elections in the country to the prayer and fasting by Nigerians and Christians in particular during the Lenten period which would soon come to an end. He said, "only the creator chooses a leader; whoever emerges as winner should be supported for the progress and unity of the country. "Let us prevail on our fellow brothers and sisters to accept the outcome of the elections, be it the seat of the President or National Assembly." The cleric further urged Christians who were observing the ongoing Lent not to go back to those worldly activities that they had

Election: Woman stabs husband to death over Buhari, Jonathan argument,.... Mass Open Grave Of Almost 100 Boko Haram Victims Found In Nigeria [Graphic Photo]

We have reported about a man who is likely to leave his wife for voting Goodluck Jonathan in the presidential election but we never saw a murder coming out of this election.Lagos State Police Command has arrested a 26-year-old pregnant woman for allegedly stabbing her husband to death during a quarrel over who would emerge winner between the Peoples Democratic Party (PDP) and All Progressives Congress (APC) presidential candidates, while voting was ongoing at Ejigbo area of the state. The incident reportedly happened at the couple’s one room apartment at 81 Military zone junction. Although accounts of the incident differ, one thing was consistent; the incident emanated from an argument over politics. According to an account, while the husband decided to vote for the PDP, his wife, simply called Onyiyechi, voted for the APC in the presidential election. This was not a problem initially, until an argument over whose choice would win ensued. Onyiyechi allegedly stabbed her hu

New Video: Linah Ft. Christian Bella – Hellow>>> Angalia hapa

Angalia hapa video mpya ya Mwanadada Linah akimshirikisha Christian Bella wimbo unaitwa ‘Hellow’

SHOW YA LADY JAY DEE NA ALI KIBA ILIVYOBAMBA KIOTA CHA M.O.G>>Angalia hapa

Mwanamuziki Lady Jay Dee akitoa burudani na Machozi Band Ijumaa ya tarehe 27 mwezi huu ndani ya kiota chake cha Mog Bar & Restaurant (Nyumbani Lounge) katika show anazofanya mara moja kwa mwezi kila Ijumaa ya mwisho wa mwezi ambapo Ijumaa hiyo alimualika Msanii machachari wa Bongo Flava Ali Kiba kwa ajili ya kukonga nyoyo za mashabiki wake ndani ya kiota hicho. Pichani juu na chini ni mashabiki wa Machozi Band wakimtunza manoti Lady Jay Dee. Umati wa mashabiki wa Machozi Band wakipata burudani kutoka kwa band hiyo inayoongozwa na Lady Jay Dee. Msanii nyota nchini, Ali Kiba akitoa burudani ya aina yake ndani ya kiota cha M.O.G Bar & Restaurant baada ya kutikia mualiko wa msanii mwezake Lady Jay Dee na kufanya Live Music bila kutumia CD na kuwafanya mashabiki kupagawa zaidi. Ali Kiba akiendelea kuwaburudisha mashabiki wake Machozi Band. Warembo walipagawajem sasa. Twende kazi hapo sasa. Mrembo akijinafasi kwa Ali Kiba. #ChekechaCheketua.......Wadada wakichizika na mauno ya Ali Ki

Barack Obama ataka amani Nigeria

  Raisi wa Marekani Barack Obama Raisi Barack Obama ametoa mwito kwa wa Nigeria kusitisha vurugu hasa kuelekea uchaguzi mkuu wa nchi hiyo mapema mwishoni mwa wiki hii. Wasi wasi wa hali ya usalama umezidi kuongezeka nchini humo wakati siku ya kupiga kura kadiri inavyokaribia ambapo wananchi wa Naijeria wanatarajiwa kupiga kura jumamosi wiki hii baada uchaguzi huo kuhairishwa mwezi uliopita kutokana na mashambulio ya kundi la Boko Haram. Rais Obama amesema kwamba Nigeria inapaswa kufanya uchaguzi ulio huru na wa haki. wanaijeria wote wanapaswa kupiga kura zao bila ya vitisho ama wasi wasi .Hivyo natoa wito kwa viongozi wote pamoja na wagombea kuzungumza na wapiga kura wao kwamba vurugu hazina nafasi katika uchaguzi wa kidemokrasia,na hawapaswi kuchochea, wasaidie au kujihusisha na vurugu zozote kabla ama baada ya uchaguzi na wakati wa kuhesabu kura. Nina waomba wanaigeria wote kueleza hisia zenu kwa amani na kuwapuuza wote wanaotoao wito wa kufanya vurugu . Wakati Rais Obma akitoa wito

Ajali zaendelea kutikisa nchini, ANGALIA PICHA ZA AJALI nyingine ya basi la SHARON iliyotokea jijini Arusha

Takribani watu 18 wamenusurika kufa jana baada ya gari la abiria lenye T 349 CXB Kampuni ya Sharoni liliokuwa linatokea Arusha kulekea dodoma kuanguka katika eneo la kisongo uwanja wa Ndege Jijini Arusha. Kwa mujibu wa abiria walikuwa ndani ya basi hilo wamesema kuwa ali hiyo imetokea baada ya dereva wa basi hilo kutaka kupita gari lililokuwa mbele yake bila kuchukua tahadhari na ndipo gari hilo lilipo acha njia kupinduka. Kwa upande wa abiria wa basi hilo aliteyejitambulisha kwa moja la Mama Latifa amesema gari hilo lilipoteza muelekeo kuwa mara baada ya gari hilo kufeli breki za nyuma. Aidha majeruhi watukio hilo wanaendelea kupatiwa matibabu katika hospital ya Rufaa Maunt Meru Jijini Arusha na wengine wameendelea na safari huku jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi wa ajali hiyo iliyotokea majira ya saa moja na nusu jana asubuhi.

MVUA YAGEUKA KERO KUBWA KWA WAKAZI WA DAR

Soko la Mchikichini, Ilala-Boma linavyoonekana kufuatia mvua za sasa Maji yalivyotapakaa soka la Sinza Afrika-Sana. Wakazi wa Mwanayamala-Mkwajuni wakitoa maji katika nyumba zao. ...Juhudi za kuondoa maji zikiendelea. Mwonekano wa nyumba za bonde la Mchikichini, Ilala-Boma. WAKATI mvua zikiendela kunyesha katika jiji la Dar es Salaam, na sehemu nyingine nchini, wakazi wake wengi wameonekana kuhangaika kupata sehemu salama za kuishi na kufanyia biashara.Mtandao huu umezungukia maeneo mbalimbali ya jiji na kukuta wakazi wa maeneo mengi wakitoa maji kwenye nyumba zao na sehemu za kufanyia biashara.   Wakiongea na mwandishi wetu, wakazi wa maeneo ya Mwanayamala-Mkwajuni maarufu kama Bondeni, wameitupia lawama kampuni ya ujenzi ya Strabag kuwa imechangia nyumba zao kuingiliwa na maji kwani mifereji iliyotengenezwa haikidhi uwezo wa kusafirisha maji kwa kasi kwani ni midogo na badala yake maji hujaa na kuelekea katika makazi yao.   Katika maeneo ya Jangwani mtandao huu