Skip to main content

Posts

Showing posts from February, 2016

Afukuzwa CCM kwa kumfanyia kampeni Lowassa

Licha ya kukiuka maadili ya umoja huo, Mwininga anadaiwa kukisaliti chama hicho wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu uliopita kwa kuwatukana viongozi wa ngazi za juu kwa njia ya mtandao. Geita. Halmashauri ya CCM Mkoa wa Geita imemvua ujumbe wa Mkutano Mkuu, Peter Mwininga baada ya kudaiwa kukiuka maadili ya Umoja wa Vijana (UVCCM). Licha ya kukiuka maadili ya umoja huo, Mwininga anadaiwa kukisaliti chama hicho wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu uliopita kwa kuwatukana viongozi wa ngazi za juu kwa njia ya mtandao. Akizungumza baada ya kikao hicho juzi, Katibu wa Siasa na Uenezi CCM mkoani hapa, Said Kalidushi alisema baada ya wajumbe wa halmashauri kuu kupokea malalamiko na mapendekezo kutoka UVCCM, waliamua kumvua nafasi ya ujumbe huo kutokana na kupungukiwa na sifa. Kalidushi alisema wakati wa kampeni Mwininga alikihujumu chama chao na kumfanyia kampeni mgombea urais wa Chadema, Edward Lowassa, huku akijua wazi kuwa ni kosa. Katibu wa UVCCM mkoani hapa, Mashaka Mshola alisema kiten

Jela miaka 30 kwa kulawiti

Ilidaiwa siku ya tukio, Ally alimlawiti mtoto huyo wa kiume mwenye umri wa miaka 16 na kumsababishia maumivu huku akijua kufanya hivyo ni kinyume cha sheria. Dar es Salaam. Mahakama ya wilaya ya Ilala leo imemhukumu Rizik Ally (25) kifungo cha miaka 30 jela baada ya kupatikana na hatia ya kulawiti mvulana wa miaka 16. Ally ambaye ni mfanyabiashara na mkazi wa Mbagala amehukumuwa kifungo hicho baada ya mahakama hiyo kuridhishwa na ushahidi wa mashahidi wanne akiwemo daktari. Akisoma hukumu hiyo jana, hakimu Flora Haule amesema mahakama yake imeridhishwa na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo dhidi ya mshtakiwa huyo. “Ally ninakuhukumu kifungo cha miaka 30 jela ili iwe fundisho kwa vijana wengie wenye tabia mbaya kama hii ya kulawiti mtoto wa kiume wakati ukijua kuwa kufanya hivyo ni kinyume cha sheria,” amesema hakimu huyo. Awali kabla ya kutolewa kwa hukumu hiyo, wakili wa serikali Ester Kyara aliiomba mahakama hiyo kutoa adhabu kali dhidi ya mshtakiwa huyo kutokana na kukithiri kw

Tazama Matokeo yote ya Kidato cha nne 2015/2016

             >>>BONYEZA HAPA>>> Kuangalia Matokeo ya QT 2015/2016    BONYEZA HAPA

Al-Shabab wasema ndio walioshambulia ndege

Kundi la wapiganaji wa Kiislamu la Al-Shabab kutoka Somalia limesema ndilo lililoshambulia ndege iliyotoboka shimo ikiwa angani mapema mwezi huu. Kupitia taarifa iliyotumwa kwa barua pepe al-Shabab wamesema shambulio hilo lilikuwa la kulipiza kisasi operesheni za kijasusi zinazoendeshwa na mataifa ya Magharibi nchini Somalia. Shimo hilo kwenye ndege hiyo lilitoboka muda mfupi baada ya ndege hiyo kupaa kutoka Mogadishu, ikiwa futi 10,000 (3,048m) juu angani. Ndege hiyo ilifanikiwa kutua kwa dharura. Ndege hiyo ya shirika la ndege la Daallo, iliyokuwa ikielekea Djibouti, ilikuwa imebeba watu karibu 60. Maafisa nchini Somalia baadaye walitoa video inayoonesha watu wawili wakimkabidhi abiria mmoja anayeshukiwa kuwa mlipuaji wa kujitolea mhanga kitu kinachoonekana kama Laptop kabla ya mlipuaji kuabiri ndege hiyo. Msemaji wa serikali anasema kuwa watu hao ndio washukiwa wakuu katika ulipuaji huo. Inasadikika kuwa mmoja kati ya watu walioleta kipakatilishi hicho

Bei ya Mafuta Yashuka Tena

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura), imetangaza bei kikomo ya mafuta, ambapo bei ya dizeli imeshuka kutoka Sh. 1,747 hadi Sh 1,600, likiwa ni punguzo la Sh. 147 kwa lita. Kadhalika, bei ya mafuta ya petroli imeshuka kwa Sh. 55, hivyo kufanya mafuta hayo kuanzia leo kuuzwa kwa bei isiyozidi Sh. 1,842 kutoka Sh. 1,898 kwa lita kama kilivyokuwa ikiuzwa mwezi uliopita. Taarifa iliyotolewa jana jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mkuu wa Ewura, Felix Ngamlagosi, ilieleza kuwa, kupungua kwa bei ya mafuta kwenye soko la ndani  kwa kiasi kikubwa kumetokana na kushuka kwa bei ya nishati hiyo katika soko la dunia na pia kushuka kwa gharama za usafarishaji na bidhaa za mafuta hayo kuja nchini. “Hakukuwa na mafuta ya taa yaliyoingizwa nchini Januari mwaka huu, hivyo Februari bei ya bidhaa hii itaendelea kuwa kama ilivyokuwa kwa Januari ambayo ni Sh. 1,699 kwa lita kwa soko la Dar es Salaam,” alisema. Ngamlagosi alisema kushuka