Skip to main content

Posts

Showing posts from May, 2016

Mke wa Trafiki Kinyogori Adaiwa Kukiri Kumuua Mumewe

MKE wa askari polisi wa kikosi cha usalama barabarani (trafiki), Sajenti Ally Salum (Kinyogori) aliyeuawa hivi karibuni, inadaiwa amekiri kuhusika kwenye mauaji hayo, akidai ilitokana na mumewe kumuacha na kuoa mke mwingine. Kamanda wa Polisi, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa mwanamke huyo anashikiliwa na polisi kwa mauaji hayo yaliyofanyika nyumbani kwa Kinyogori, Mkuranga mkoani Pwani. Wakati huo huo, Kamanda Sirro amezungumzia pia mauaji ya Anathe Msuya yaliyofanyika hivi karibuni Kigamboni na kusema polisi inaendelea kumtafuta msichana wa kazi za nyumbani aliyetoroka siku moja kabla ya kifo cha mwanamke huyo. Anayetuhumiwa kuua mumewe  Akizungumza na waandishi wa habari jana kuhusu matukio mbalimbali ya uhalifu yaliyojitokeza jijini Dar es Salaam, Sirro alisema katika mahojiano ya awali mke wa Kinyogori amekiri kuhusika. Kwa mujibu wa kamanda, mwanamke huyo ambaye hata hivyo hakutaja jina lake

Soma Habari Zote Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne May 31

Soma Habari Zote Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi May 28

EXCLUSIVE: Aunty Ezekiel Kaelezea Siku Mose Iyobo Alipohisi Mtoto Sio Wake

Mwigizaji Aunty Ezekiel amekaa kwenye Exclusive ya AyoTV na kuelezea vitu kadhaa kwenye mapenzi yake na Dancer wa Diamond Platnumz  Mose Iyobo ambapo miongoni mwa alivyoongelea ni pamoja na siku ambayo Mose alihisi ujauzito aliokua nao Aunty sio wa mtoto wake. ‘Kwanza Mose Iyobo aliniambia niitoe hii mimba nilipomuuliza kwanini akasema najua wewe Aunty Ezekiel huwezi kuzaa na mimi, akaniambia hajajipanga sababu ana mtoto mwingine, nilimwambia hii mimba ni yangu na kila afanye maisha yake kama ni hivyo….‘ – Aunty Ezekiel

MOURINHO NI MENEJA MPYA MAN UNITED!---RASMI

José Mourinho ndie Meneja mpya wa Manchester United kwa Msimu wa 2016/17 baada ya kusaini Mkataba wa Miaka Mitatu ambao pia unaweza kumuweka hadi Mwaka 2020. José, Raia wa Ureno mwenye Miaka 53 na ambae ametwaa Makombe 22 tangu 2003, amefundisha Klabu kadhaa kubwaa Ulaya na kutwaa Mtaji katika Nchi 4 tofauti (Portugal, England, Italy na Spain) ikiwa pamoja na kutwaa UEFA CHAMPIONZ LIGI, mara 2 akiwa na FC Porto 2004 na Inter Milan 2010. Akitangaza rasmi uteuzi huu, Makamu Mwenyekiti Mtendaji wa Man United Ed Woodward, alisema: “Jose ni Meneja Bora kabisa kwenye Gemu hivi sasa. Ametwaa Mataji na kuhamasisha Wachezaji katika Nchi kadhaa Ulaya na pia anaijua Ligi Kuu England nje ndani ambako ametwaa Ubingwa mara 3! Namkaribisha Manchester United!” Nae José Mourinho amesema: "Kuwa Meneja wa Manchester United ni heshima spesho katika Gemu. Ni Klabu inayojulikana na inayopendwa Dunia nzima. Kuna kitu cha ajabu na mapenzi ambacho Klabu nyingine yeyote hawana!” Aliongeza: “Sik

Wadaiwa vyuo vikuu kukamatwa kirahisi

WAKATI serikali ikipanga kuifanyia marekebisho Sheria ya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), Bunge limependekeza wanafunzi wanaonufaika na mikopo hiyo wasipewe vyeti vyao hadi pale watakaporejesha mikopo.  Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Dk Joyce Ndalichako akiwasilisha hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya wizara yake Bungeni jana.  Akiwasilisha bungeni makadirio ya mapato na matumizi ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2016/17 mjini hapa jana, Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolijia na Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako, alisema serikali itaifanyia marekebisho Sheria ya Bodi ya Mikopo ili kuongeza kasi ya urejeshwaji wa mikopo.  Profesa Ndalichako alisema watalazimika kuifanyia marekebisho sheria hiyo kwa kuwa kiwango cha urejeshwaji wa mikopo bado hakiridhishi.  Alisema hali hiyo inasababishwa na kuwapo kwa changamoto za kutokuwapo kwa mikakati thabiti ya ufuatiliaji wa wakopaji, udhaifu katika Sheria ya Muundo wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa

Soma Habari zote Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya May 24