Skip to main content

YANGA YAPEWA UBINGWA LIGI KUU YA VODACOM 2014/2015

leooo 

Yanga Bingwa 2015/2016!! Hizi ni baadhi ya headlines kwenye kurasa za michezo.. haikumaanisha kwamba matokeo ya mwisho yalikuwa yameamua hivyo, ila wanaspoti walipiga hesabu ya pointi ambazo yatari YANGA walikuwa wamejikusanyia mpaka mechi yao ya mwisho, hii ya leo ambayo Yanga wamekutana na Polisi Morogoro tayari imetoa matokeo.

Yanga imefikisha jumla ya pointi 55 ambazo haziwezi kufikiwa na timu nyingine yoyote inayoshiriki ligi kuu msimu huu, kwa matokeo hayo basi Yanga wanakuwa mabingwa wa Ligi hiyo.

Mechi hiyo kati ya Yanga na Polisi Moro ilikuwa ikipigwa katika Uwanja wa Taifa Dar.. mechi imekamilika kwa Yanga kutoka kifua mbele kwa goli 4-1.

Hamis Tambwe leo aliweza kuing’arisha Yanga baada ya kupachika magoli matatu ambapo goli la kwanza alifunga dakika ya 40 kufuatia krosi ya Saimon Msuva, goli la pili alilifunga dakika ya 53 na goli la mwisho alifunga baada ya kupokea cross kutoka kwa Mrisho Ngassa.

Msuva alikamilisha idadi ya mabao kwa kupiga bao la nne ambapo baadae dakika ya 83 Polisi walishinda bao la kufutia machozi kupitia kwa Bantu Admini aliyepiga shuti kali akiwa nje ya 18.

Ligi kuu Tanzania Bara inatarajiwa kukamilika mwisho wa wiki katika mechi za kukamilisha ratiba ya ligi hiyo kwa msimu huu.

 Mshambuliaji wa Yanga Amissi Tambwe akishangilia baada ya kufunga bao la kwanza dhidi ya Polisi Moro kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar.

Wachezaji wa timu ya Yanga.










Comments

Popular posts from this blog

MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA SABA 2015 YOTE HAYA HAPA

Angalia yote hapa NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA PSLE-2015 EXAMINATION RESULT ARUSHA DAR ES SALAAM DODOMA IRINGA KAGERA KIGOMA KILIMANJARO LINDI MARA MBEYA MOROGORO MTWARA MWANZA PWANI RUKWA RUVUMA SHINYANGA SINGIDA TABORA TANGA MANYARA GEITA KATAVI NJOMBE SIMIYU   

VIDEO MPYA: AMANI - KIZUNGU ZUNGU

Angalia hapa

HUYU NDIE MWANAUME"[SHOGA] MWENYE MAKALIO MAKUBWA KULIKO WOTE DUNIANI,KAAMUA KUPOST HIZI PICHA INSTAGRAM.

Kutana na mwanaume mwenye makalio makubwa kama mwanamke.Kwa jina anaitwa Micah,ni mwanaume ambaye hipsi na makalio yake zinazidi hata zile za wanawake huwezi kuamini hebu tazama hapa utakubali tu mwenyewe.