Skip to main content

Arsenal yasajili nyota wa Brazil.





Klabu ya Arsenal iko mbioni kukamilisha usajili wa nyota raia wa Brazil Gabriel Paulista toka kwenye klabu ya Villareal ya nchini Hispania .

Usajili huu utakamilika siku chache zijazo baada ya mchezaji huyo kupata kibali ch akufanyia kazi nchini England kulingana na sheria za kazi kwa raia wanaotoka nje ya umoja wa ulaya .

Beki huyo mwenye umri wa miaka 24 anatarajiwa kukamilisha vipimo vya afya hii leo (jumatatu) na atakamilisha usajili wake baada ya hapo .


Gabriel Paulista atajiunga na Arsenal muda wowote kuanzia sasa.

Awali kulikuwa na hofu kuwa Paulista angenyimwa kibali cha kufanyia kazi kwa kuwa hajacheza mechi zozote za kimataifa lakini hiyo haitakuwa shida kwani ameichezea klabu ya Villareal kwa muda mrefu na amekidhi vigezo vya kupata kibali cha kufanyia kazi nchini humo .

Kocha wa Arsenal Arsene Wenger amethibitisha hili ambapo amesema kuwa dili la kumsajili beki huyo litakamilika muda wowote kuanzia sasa .

Paulista aligana na wachezaji wenzie wa Villareal dakika chache kabla ya mchezo dhidi ya Levante kwenye ligi ya Hispania huku pia akitumia fursa hiyo kuagana na mashabiki.


Mshambuliaji wa Costa Rica Joel Campbell ameruhusiwa kujiunga na Villareal kwa mkopo mpaka mwisho wa msimu huu kama sehemu ya usajili wa Gabriel Paulista.

Katika mchakato wa kumsajili Paulista Arsenal imemruhusu mshambuliaji raia wa Costa Rica Joel Campbell kujiunga na Villareal kwa muda wote uliobaki wa msimu huu .

Comments

Popular posts from this blog

MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA SABA 2015 YOTE HAYA HAPA

Angalia yote hapa NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA PSLE-2015 EXAMINATION RESULT ARUSHA DAR ES SALAAM DODOMA IRINGA KAGERA KIGOMA KILIMANJARO LINDI MARA MBEYA MOROGORO MTWARA MWANZA PWANI RUKWA RUVUMA SHINYANGA SINGIDA TABORA TANGA MANYARA GEITA KATAVI NJOMBE SIMIYU   

HUYU NDIE MWANAUME"[SHOGA] MWENYE MAKALIO MAKUBWA KULIKO WOTE DUNIANI,KAAMUA KUPOST HIZI PICHA INSTAGRAM.

Kutana na mwanaume mwenye makalio makubwa kama mwanamke.Kwa jina anaitwa Micah,ni mwanaume ambaye hipsi na makalio yake zinazidi hata zile za wanawake huwezi kuamini hebu tazama hapa utakubali tu mwenyewe.

Matokeo ya kidato cha pili mwaka 2015: Zanzibar

MATOKEO YA MITIHANI YA KIDATO CHA PILI KWA MWAKA 2015 KIWILAYA MJINI MAGHARIBI KUSINI UNGUJA KATI KASKAZINI "A" KASKAZINI "B" MKOANI CHAKE CHAKE WETE MICHEWENI SKULI ZA BINAFSI TANBIHI: KWA UFAFANUZI WA SUALA LOLOTE LINALOHUSU MATOKEO YA MITIHANI TAFADHALI WASILIANA NA OFISI ZA BARAZA LA MITIHANI ZANZIBAR UNGUJA NA PEMBA - AHSANTENI. Source:    Ministry of Education and Vocational Training - Zanzibar Angalia Matikeo ya kidato cha pili bara hapa chini Posted by Maarifa & FIKRA Yakinifu on  Friday, January 15, 2016