Skip to main content

Wakerwa shilingi kushuka thamani

Tanzania Sh.



                                                                           VS
U.S Dollar

Dar es Salaam. Wasomi nchini wamezungumzia kuhusu kupanda kwa thamani ya Dola ya Marekani dhidi ya Shilingi ya Tanzania na kusema kunasababishwa na kuongezeka kwa uagizaji wa bidhaa kutoka nje na kusababisha fedha nyingi kutafutwa ili kulipia bidhaa hizo.


Bidhaa hizo ambazo huingizwa nchini hulipiwa kwa dola, hivyo ukusanyaji fedha nyingi huhitajika ili kukidhi bei zinazoelekezwa na wafanyabiashara wa nje. Hii husababisha kuwa na uhitaji mkubwa wa dola kuliko shilingi.


Thamani ya shilingi dhidi ya Dola ya Marekani jana iliuzwa kwa Sh1,813 katika maduka ya kubadilishia fedha. Hata hivyo kwa viwango vya Benki Kuu (BoT), dola iliuzwa kwa Sh1,768.


Mkuu wa Shule ya Biashara ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDBS), Profesa Winieaster Andasom alisema taifa linakabiliwa na tatizo kubwa la uagizaji bidhaa nyingi kutoka nje kuliko zile zinazouzwa nje.


Alisema ili uchumi wa taifa ukue na thamani ya shilingi iwe na nguvu, lazima Watanzania waongeze uwezo wa kuuza bidhaa zao nje na kwa fedha za kigeni. Aliongeza kuwa kitendo cha uagizaji bidhaa kwa wingi kutoka nje kinafanya matumizi ya shilingi kudidimia na kupoteza thamani.


Aliitaka Serikali kuagiza bidhaa muhimu tu kama mashine, mafuta na zana ambazo hazizalishwi nchini. Lakini bidhaa nyingine kama mazao ya chakula na sukari, alisema hamna haja ya kuagiza kutoka nje. Profesa Andasom pia alibainisha kuwa thamani ya shilingi inaporomoka, kutokana na mfumuko mkubwa wa bei.


Alisema wananchi ndiyo waathirika wakubwa kunapotokea na mfumuko wa bei na maovu mengi huongezeka katika jamii.


Naye Profesa Humphrey Moshi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), alisisitiza kuwa uagizaji wa bidhaa nje ya nchi kuliko zinazozalishwa nchini kunayanufaisha mataifa mengine kwa sababu wanauza kwa thamani ya fedha yao.


Profesa Moshi aliongeza kuwa njia pekee ya kutatua tatizo hilo ni kuweka mikakati ya kuboresha kilimo ili mazao mengi yauzwe nje. Alisema ni muhimu kuwa na kilimo kisichotegemea mvua, badala yake kuwe na kilimo cha umwagiliaji.


Waziri wa Fedha na Uchumi, Saada Mkuya alikiri kupanda kwa Dola ya Kimarekani na kusema kuwa, “hili liko wazi kwamba bidhaa zinazoingizwa nchini kutoka nje ya nchi ni nyingi kuliko zinazozalishwa nchini kwenda nje ya nchi.”


Aliongeza: “Kinachotakiwa ili dola isiendelee kupaa ni kuhakikisha tunazalisha bidhaa zenye ubora ili ziende kwa wingi nje ya nchi na hapo tutaweza kupambana na kupanda kwa dola.”

Comments

Popular posts from this blog

HUYU NDIE MWANAUME"[SHOGA] MWENYE MAKALIO MAKUBWA KULIKO WOTE DUNIANI,KAAMUA KUPOST HIZI PICHA INSTAGRAM.

Kutana na mwanaume mwenye makalio makubwa kama mwanamke.Kwa jina anaitwa Micah,ni mwanaume ambaye hipsi na makalio yake zinazidi hata zile za wanawake huwezi kuamini hebu tazama hapa utakubali tu mwenyewe.

MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA SABA 2015 YOTE HAYA HAPA

Angalia yote hapa NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA PSLE-2015 EXAMINATION RESULT ARUSHA DAR ES SALAAM DODOMA IRINGA KAGERA KIGOMA KILIMANJARO LINDI MARA MBEYA MOROGORO MTWARA MWANZA PWANI RUKWA RUVUMA SHINYANGA SINGIDA TABORA TANGA MANYARA GEITA KATAVI NJOMBE SIMIYU   

Fasihi simulizi na Chimbuko la Riwaya

                                                                    Fasihi simulizi na Andishi HISTORIA YA FASIHI SIMULIZI YA KIAFRIKA KWA MTAZAMO WA NADHARI ZA UTANDAWAZI, UTAIFA NA HULUTISHI . Utangulizi Fasihi simulizi kwa mujibu wa Mlokozi (1996), ni fasihi inayotungwa au kubuniwa kichwani na kuwasilishwa kwa hadhira kwa njia ya mdomo na vitendo bila kutumia maandishi. Hivyo fasihi simulizi inafungamana   na muktadha au mazingira fulani ya kijamii na kutawaliwa na muingiliano wa mambo kama vile Fanani, Hadhira, Fani inayotendwa, Tukio, Mahali pamoja na Wakati wa utendaji.             Balisidya (1983) anasema fasihi simulizi ni aina ya fasihi ambayo hutumia mdomo katika kuumbwa, kuwasilishwa na kusambazwa kwa wasikilizaji na watumiaji wake. Mt...