Skip to main content

Barack Obama ataka amani Nigeria

 
Raisi wa Marekani Barack Obama

Raisi Barack Obama ametoa mwito kwa wa Nigeria kusitisha vurugu hasa kuelekea uchaguzi mkuu wa nchi hiyo mapema mwishoni mwa wiki hii.

Wasi wasi wa hali ya usalama umezidi kuongezeka nchini humo wakati siku ya kupiga kura kadiri inavyokaribia ambapo wananchi wa Naijeria wanatarajiwa kupiga kura jumamosi wiki hii baada uchaguzi huo kuhairishwa mwezi uliopita kutokana na mashambulio ya kundi la Boko Haram.

Rais Obama amesema kwamba Nigeria inapaswa kufanya uchaguzi ulio huru na wa haki.

wanaijeria wote wanapaswa kupiga kura zao bila ya vitisho ama wasi wasi .Hivyo natoa wito kwa viongozi wote pamoja na wagombea kuzungumza na wapiga kura wao kwamba vurugu hazina nafasi katika uchaguzi wa kidemokrasia,na hawapaswi kuchochea, wasaidie au kujihusisha na vurugu zozote kabla ama baada ya uchaguzi na wakati wa kuhesabu kura.

Nina waomba wanaigeria wote kueleza hisia zenu kwa amani na kuwapuuza wote wanaotoao wito wa kufanya vurugu .

Wakati Rais Obma akitoa wito huo Joto la uchaguzi linazidi kupamba moto nchini Nigeria.

Mvutano mkali upo kati ya rais Goodluck Jonathan wa chama tawala cha PDP na mgombea wa upinzani Jenerali Muhhamadu Buhari wa APC. Wananchi wa Nigeria watapiga kura siku ya Jumamosi kuchagua mtu atakayewaongioza kwa miaka minne ijayo.
 
Chano BBC

Comments

Popular posts from this blog

MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA SABA 2015 YOTE HAYA HAPA

Angalia yote hapa NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA PSLE-2015 EXAMINATION RESULT ARUSHA DAR ES SALAAM DODOMA IRINGA KAGERA KIGOMA KILIMANJARO LINDI MARA MBEYA MOROGORO MTWARA MWANZA PWANI RUKWA RUVUMA SHINYANGA SINGIDA TABORA TANGA MANYARA GEITA KATAVI NJOMBE SIMIYU   

HUYU NDIE MWANAUME"[SHOGA] MWENYE MAKALIO MAKUBWA KULIKO WOTE DUNIANI,KAAMUA KUPOST HIZI PICHA INSTAGRAM.

Kutana na mwanaume mwenye makalio makubwa kama mwanamke.Kwa jina anaitwa Micah,ni mwanaume ambaye hipsi na makalio yake zinazidi hata zile za wanawake huwezi kuamini hebu tazama hapa utakubali tu mwenyewe.

Matokeo ya kidato cha pili mwaka 2015: Zanzibar

MATOKEO YA MITIHANI YA KIDATO CHA PILI KWA MWAKA 2015 KIWILAYA MJINI MAGHARIBI KUSINI UNGUJA KATI KASKAZINI "A" KASKAZINI "B" MKOANI CHAKE CHAKE WETE MICHEWENI SKULI ZA BINAFSI TANBIHI: KWA UFAFANUZI WA SUALA LOLOTE LINALOHUSU MATOKEO YA MITIHANI TAFADHALI WASILIANA NA OFISI ZA BARAZA LA MITIHANI ZANZIBAR UNGUJA NA PEMBA - AHSANTENI. Source:    Ministry of Education and Vocational Training - Zanzibar Angalia Matikeo ya kidato cha pili bara hapa chini Posted by Maarifa & FIKRA Yakinifu on  Friday, January 15, 2016