Skip to main content

WOLPER ANASWA LIVE FREEMASON>> Angalia hapa ilivyokuwa

Mshtuko! Staa wa sinema za Kibongo, Jacqueline Wolper Massawe ameibua maswali kwa mashuhuda walimuona ‘live’ akiingia kwenye hekalu la watu wa Jamii ya Siri (Secret Society) ya Freemasons yenye nguvu duniani inayohusishwa na imani za kishetani.

 Staa wa sinema za Kibongo, Jacqueline Wolper Massawe akiingia kwenye hekalu ilo.
TUJIUNGE MTAA WA SOKOINE
Tukio hilo lililoibua kizaazaa kwa mashuhuda waliomuona Wolper, lilijiri juzikati, mishale ya jioni kwenye hekalu hilo lililopo Mtaa wa Sokoine mkabala na Hoteli ya Hyatt Regency, The Kilimanjaro jijini Dar jirani na Benki Kuu ya Tanzania (BoT).
SIMU ZAMIMINIKA
Likiwa kwenye majukumu ya kusaka habari kama kawaida yake, gazeti hili lilipokea simu kadhaa kutoka kwa mashuhuda hao wakiwataka wanahabari wetu kuwahi eneo la tukio.
Kufuatia umbali waliokuwa mapaparazi wetu, ilibidi kuwaomba mashuhuda hao ‘kumfotoa’ picha ambapo mmoja wao alifanya hivyo na kuziwasilisha kwenye meza ya gazeti hili.
...akitoka.
ALINASWAJE?
Akidadavua mazingira aliyonaswa Wolper, shuhuda huyo alikuwa na haya ya kusema:
“Kwanza mwanzoni hatukumjua kama ni Wolper lakini kuna dada ambaye anamjua vizuri na ni shabiki wake mkubwa ndiye aliyetuhakikishia kuwa ni Jacqueline (Wolper).
“Kuna waliomuona akiingia. Nilipofika mimi nilimkuta getini anatoka. Walisema hakukaa muda mrefu kwani alitumia dakika kadhaa kisha akatoka na kwenda kwenye gari lake aina ya Prado (Toyota) alilopaki mbali kidogo na lango hilo,” alisema shuhuda huyo kwa sharti la kutotajwa jina na kuongeza:
“Baada ya hapo alitoka nduki maana nzi (watu) walikuwa wameanza kumjalia na kulizingira gari lake.”
WOLPER AJITETEA
Baada ya kuzikagua picha za Wolper akiwa katika mazingira hayo na kujiridhisha kuwa ni yeye, gazeti hili lilimbana mwigizaji huyo ambapo alijitetea:
...akiwa getini.
“Jamani nilikuwa sina hili wala lile. Kuna jengo nilikuwa nalitafuta ndiyo nikajikuta nimetokea maeneo hayo.
“Mimi mwenyewe nilishtuka kuona watu wananiangalia sana kumbe ndiyo nikagundua nipo kwenye lango la Freemasons.”
Risasi Jumamosi: Mbona kuna mashuhuda walikuona wakati unaingia na wakati unatoka?
Wolper: Unajua mimi sikuona kibao chao lakini sikuingia kabisa hadi kule ndani.
Risasi Jumamosi: Lakini kuna madai kwamba wewe ni mwanachama. Unasemaje?
Wolper: Mimi siyo Freemasons, nakumbuka kuna siku watu walinifuata wakaniambia nijiunge Freemasons nitakuwa na mafanikio lakini sijakubaliana nao.
TUJIKUMBUSHE
Mwaka 2012 wakati wa kifo cha aliyekuwa mwigizaji mkubwa Bongo, marehemu Steven Kanumba ‘The Great’ kuliibuka madai ya baadhi ya wasanii ambao ilisemekana ni ‘memba’ wa Freemasons.
Staa wa sinema za Kibongo, Jacqueline Wolper Massawe.
Mbali na Kanumba, wengine waliotajwa kwenye listi hiyo mwaka huo alikuwepo Wolper na mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ ambaye madai hayo yamekuwa yakiendelea kumganda huku wengi wakiwa na imani potofu kuwa ukijiunga na jamii hiyo unapata utajiri wa ghafla.

Comments

  1. Duuh hizi habari zimeniacha mdomo wazi ndugu mwandishi. Tupatie habari nyingine tena kemkem zenye kusisimua vinywa vya hadhira wako nikiwemo mimi.
    Ahsante!

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA SABA 2015 YOTE HAYA HAPA

Angalia yote hapa NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA PSLE-2015 EXAMINATION RESULT ARUSHA DAR ES SALAAM DODOMA IRINGA KAGERA KIGOMA KILIMANJARO LINDI MARA MBEYA MOROGORO MTWARA MWANZA PWANI RUKWA RUVUMA SHINYANGA SINGIDA TABORA TANGA MANYARA GEITA KATAVI NJOMBE SIMIYU   

HUYU NDIE MWANAUME"[SHOGA] MWENYE MAKALIO MAKUBWA KULIKO WOTE DUNIANI,KAAMUA KUPOST HIZI PICHA INSTAGRAM.

Kutana na mwanaume mwenye makalio makubwa kama mwanamke.Kwa jina anaitwa Micah,ni mwanaume ambaye hipsi na makalio yake zinazidi hata zile za wanawake huwezi kuamini hebu tazama hapa utakubali tu mwenyewe.

Matokeo ya kidato cha pili mwaka 2015: Zanzibar

MATOKEO YA MITIHANI YA KIDATO CHA PILI KWA MWAKA 2015 KIWILAYA MJINI MAGHARIBI KUSINI UNGUJA KATI KASKAZINI "A" KASKAZINI "B" MKOANI CHAKE CHAKE WETE MICHEWENI SKULI ZA BINAFSI TANBIHI: KWA UFAFANUZI WA SUALA LOLOTE LINALOHUSU MATOKEO YA MITIHANI TAFADHALI WASILIANA NA OFISI ZA BARAZA LA MITIHANI ZANZIBAR UNGUJA NA PEMBA - AHSANTENI. Source:    Ministry of Education and Vocational Training - Zanzibar Angalia Matikeo ya kidato cha pili bara hapa chini Posted by Maarifa & FIKRA Yakinifu on  Friday, January 15, 2016