Skip to main content

Lowassa Apata Wakati Mgumu Mkoani Mara Ambako ni Nyumbani kwa Wassira........ Maelfu ya Wananchi Wazuia Msafara Wake Wakitaka Wamuone

Waziri mkuu wa zamani Mh.Edward Lowasa aliyeko kanda ya ziwa kutafuta wadhamini amepata wakati  mgumu alipowasili mkoani Mara baada ya makundi ya wananchi wakiwemo vijana,wanawake na watoto   kumfuata kila alikokwenda wakitaka wapewe nafasi ya kumueleza kero zao jambo lililosababisha  zoezi la kumdhamini kuwa gumu licha ya kufanikiwa kwa kiasi kikubwa.
 
Heka heka za wananchi kutaka kuzuia msafara wa Mh.Lowasa zilianza mapema asubuhi wakati  anawasili kwenye uwanja wa ndege wa musoma ambapo vijana walizuia msafara wake kutoka kwenye  uwanja huo wakitaka wapewe nafasi ya kuonana naye.

Baada ya waratibu wa msafara huo kufanya kazi ya ziada ya kufanikiwa kutatua changamoto hiyo Mh.Lowasa aliekea katika wilaya ya Bunda na licha ya kusimamishwa na wananchi njiani hali  ilikuwa ngumu zaidi katika ofisi ya CCM wilaya ya  hiyo kutokana na watu kujitokeza kwa wingi.

Hata hivyo pamoja na maelfu ya wananchi hao wanaounga mkono safari ya matumaiani kuwa na shauku ya kumueleza Mh.Lowasa shida zao alishindwa kuwasikiliza  kutokana na kubanwa na kanuni   na aliwaomba kuwa watulivu na kuendelea kuiombea kheri safari ya matumaini.

Mh.Lowasa akiwa katika mkoa wa Mara  amepata idadi kubwa ya wadhaamini pia amefika  nyumbani kwa hayati baba wa taifa Mwalimu Nyerere na kupewa  baraka,  kisha kuweka shada la maua kwenye kaburi na pia  ametembelea wilaya ya Tarime na Musoma.

Mh.Lowassa ambaye ameshatembelea mikoa ya Mwanza Geita,Zanzibar na Pemba anaendelea na ziara yake ya kutafuta wadhamini katika mkoa wa Simiyu.  
 Maelfu  ya  Wananchi  wakiwa  wameuzuia  Msafara  wa  Lowassa  wakishinikiza  kumuona, hali  iliyowalazimu Polisi  na waratibu  wa  msafara  ya  kutumia  njia  mbadala  kutatua  changamoto  hiyo
 
Mh. Lowassa  alipotembelea  Kaburi  la  Baba  wa  Taifa, Hayati Mwl. J.K. Nyerere

Comments

Popular posts from this blog

HUYU NDIE MWANAUME"[SHOGA] MWENYE MAKALIO MAKUBWA KULIKO WOTE DUNIANI,KAAMUA KUPOST HIZI PICHA INSTAGRAM.

Kutana na mwanaume mwenye makalio makubwa kama mwanamke.Kwa jina anaitwa Micah,ni mwanaume ambaye hipsi na makalio yake zinazidi hata zile za wanawake huwezi kuamini hebu tazama hapa utakubali tu mwenyewe.

MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA SABA 2015 YOTE HAYA HAPA

Angalia yote hapa NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA PSLE-2015 EXAMINATION RESULT ARUSHA DAR ES SALAAM DODOMA IRINGA KAGERA KIGOMA KILIMANJARO LINDI MARA MBEYA MOROGORO MTWARA MWANZA PWANI RUKWA RUVUMA SHINYANGA SINGIDA TABORA TANGA MANYARA GEITA KATAVI NJOMBE SIMIYU   

New Video: Matunzo Zero Unit Ft.Young Killer – Furaha Yetu

Angalia hapa video mpya ya Matunzo zero unit wakimshirikisha Young Killer wimbo unaitwa ‘Furaha Yetu’ Angalia hapa  na  Download