Skip to main content

Jela miaka 30 kwa kulawiti



Ilidaiwa siku ya tukio, Ally alimlawiti mtoto huyo wa kiume mwenye umri wa miaka 16 na kumsababishia maumivu huku akijua kufanya hivyo ni kinyume cha sheria.

Dar es Salaam. Mahakama ya wilaya ya Ilala leo imemhukumu Rizik Ally (25) kifungo cha miaka 30 jela baada ya kupatikana na hatia ya kulawiti mvulana wa miaka 16.

Ally ambaye ni mfanyabiashara na mkazi wa Mbagala amehukumuwa kifungo hicho baada ya mahakama hiyo kuridhishwa na ushahidi wa mashahidi wanne akiwemo daktari.

Akisoma hukumu hiyo jana, hakimu Flora Haule amesema mahakama yake imeridhishwa na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo dhidi ya mshtakiwa huyo.

“Ally ninakuhukumu kifungo cha miaka 30 jela ili iwe fundisho kwa vijana wengie wenye tabia mbaya kama hii ya kulawiti mtoto wa kiume wakati ukijua kuwa kufanya hivyo ni kinyume cha sheria,” amesema hakimu huyo.

Awali kabla ya kutolewa kwa hukumu hiyo, wakili wa serikali Ester Kyara aliiomba mahakama hiyo kutoa adhabu kali dhidi ya mshtakiwa huyo kutokana na kukithiri kwa vitendo hivyo.

“Naiomba mahakama hii itoe adhabu kali dhidi ya mshtakiwa huyu kutokana na kukithiri kwa vitendo vya kulawiti watoto ambavyo huwaletea madhara makubwa watoto hawa ikiwemo kuathirika kisaikolojia,” alidai Kyara.

Awali akisoma hati ya mashtaka, Kyara alidai mshtakiwa alitenda kosa hilo Desemba, 2011 katika eneo la Kariakoo.

Ilidaiwa siku ya tukio, Ally alimlawiti mtoto huyo wa kiume mwenye umri wa miaka 16 na kumsababishia maumivu huku akijua kufanya hivyo ni kinyume cha sheria.

Comments

Popular posts from this blog

MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA SABA 2015 YOTE HAYA HAPA

Angalia yote hapa NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA PSLE-2015 EXAMINATION RESULT ARUSHA DAR ES SALAAM DODOMA IRINGA KAGERA KIGOMA KILIMANJARO LINDI MARA MBEYA MOROGORO MTWARA MWANZA PWANI RUKWA RUVUMA SHINYANGA SINGIDA TABORA TANGA MANYARA GEITA KATAVI NJOMBE SIMIYU   

HUYU NDIE MWANAUME"[SHOGA] MWENYE MAKALIO MAKUBWA KULIKO WOTE DUNIANI,KAAMUA KUPOST HIZI PICHA INSTAGRAM.

Kutana na mwanaume mwenye makalio makubwa kama mwanamke.Kwa jina anaitwa Micah,ni mwanaume ambaye hipsi na makalio yake zinazidi hata zile za wanawake huwezi kuamini hebu tazama hapa utakubali tu mwenyewe.

Matokeo ya kidato cha pili mwaka 2015: Zanzibar

MATOKEO YA MITIHANI YA KIDATO CHA PILI KWA MWAKA 2015 KIWILAYA MJINI MAGHARIBI KUSINI UNGUJA KATI KASKAZINI "A" KASKAZINI "B" MKOANI CHAKE CHAKE WETE MICHEWENI SKULI ZA BINAFSI TANBIHI: KWA UFAFANUZI WA SUALA LOLOTE LINALOHUSU MATOKEO YA MITIHANI TAFADHALI WASILIANA NA OFISI ZA BARAZA LA MITIHANI ZANZIBAR UNGUJA NA PEMBA - AHSANTENI. Source:    Ministry of Education and Vocational Training - Zanzibar Angalia Matikeo ya kidato cha pili bara hapa chini Posted by Maarifa & FIKRA Yakinifu on  Friday, January 15, 2016