Skip to main content

Ibrahimovic ajiita ‘Mungu’ wa Man United


Manchester, England. Kwa waumini wa dini mbalimbali duniani, watashangazwa na kauli ya mshambuliaji wa Manchester United, Zlatan Ibrahimovic.

Mshambuliaji huyo raia wa Sweden aliyetua Manchester United msimu huu akiwa mchezaji huru na kulakiwa kwa kejeli na mchezaji wa zamani wa klabu hiyo, Eric Cantona amejibu mapigo kwa kauli inayoshangaza.

Alisema kama Cantona ni Mfalme wa United, yeye ataondoka klabu hiyo ya Old Trafford akiwa ‘mungu’ wa klabu hiyo.

Cantona alimweleza Ibrahimovic kuwa anaweza kuwa mwana mfalme Old Trafford, kamwe hawezi kuyafikia mafanikio yake, yeye ni mfalme.

Lakini, Ibrahimiovic alijibu kwamba mashabiki wa klabu hiyo wasubiri waone na yuko tayari kumziba mdomo Mfaransa huyo mwenye makeke.

Alisema: “Ninamzimia Cantona. Nilisikia yale aliyoyasema. Lakini, siwezi kuwa mfalme wa Manchester. Nitakuwa ‘mungu’ wa Manchester,” limeeleza gazeti la Aftonbladet la Sweden.

Ibrahimovic aliyetoa kauli tata wakati akiondoka Paris Saint-Germain aliongeza: “Nilikwenda kule mfalme, niliondoka nikiwa mkongwe.”

Nyota huyo wa zamani wa Barcelona alitarajiwa kuanza mazoezi na klabu hiyo baada ya kusaini mkataba wa mwaka mmoja.

Alieleza dhamira yake ya kuongeza mataji kwenye kabati lake akiwa nayo ya Uholanzi, Hispania, Italia na Ufaransa.

Cantona alimweleza Ibrahimovic alipojiunga na United kuwa ni chaguo sahihi alilolifanya katika maisha yake, lakini kamwe hawezi kuyafikia mafanikio yake.

“Ninao ujumbe maalumu kwake, Zlatan, ameamua kutua hapa, kuvaa jezi nyekundu. Ni chaguo sahihi alilofaya katika maisha yake.

Credit: Mwananchi

Popular posts from this blog

HUYU NDIE MWANAUME"[SHOGA] MWENYE MAKALIO MAKUBWA KULIKO WOTE DUNIANI,KAAMUA KUPOST HIZI PICHA INSTAGRAM.

Kutana na mwanaume mwenye makalio makubwa kama mwanamke.Kwa jina anaitwa Micah,ni mwanaume ambaye hipsi na makalio yake zinazidi hata zile za wanawake huwezi kuamini hebu tazama hapa utakubali tu mwenyewe.

MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA SABA 2015 YOTE HAYA HAPA

Angalia yote hapa NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA PSLE-2015 EXAMINATION RESULT ARUSHA DAR ES SALAAM DODOMA IRINGA KAGERA KIGOMA KILIMANJARO LINDI MARA MBEYA MOROGORO MTWARA MWANZA PWANI RUKWA RUVUMA SHINYANGA SINGIDA TABORA TANGA MANYARA GEITA KATAVI NJOMBE SIMIYU   

Fasihi simulizi na Chimbuko la Riwaya

                                                                    Fasihi simulizi na Andishi HISTORIA YA FASIHI SIMULIZI YA KIAFRIKA KWA MTAZAMO WA NADHARI ZA UTANDAWAZI, UTAIFA NA HULUTISHI . Utangulizi Fasihi simulizi kwa mujibu wa Mlokozi (1996), ni fasihi inayotungwa au kubuniwa kichwani na kuwasilishwa kwa hadhira kwa njia ya mdomo na vitendo bila kutumia maandishi. Hivyo fasihi simulizi inafungamana   na muktadha au mazingira fulani ya kijamii na kutawaliwa na muingiliano wa mambo kama vile Fanani, Hadhira, Fani inayotendwa, Tukio, Mahali pamoja na Wakati wa utendaji.             Balisidya (1983) anasema fasihi simulizi ni aina ya fasihi ambayo hutumia mdomo katika kuumbwa, kuwasilishwa na kusambazwa kwa wasikilizaji na watumiaji wake. Mt...