Skip to main content

Mapigano yazuka Kidal, Mali

Wapiganaji kutoka moja ya makundi yanayopigana kwenye mji wa Kidal,Mali
Kundi la wanamgambo la Tuareg linaloungwa mkono na Serikali linasemekana kuchukua udhibiti wa mji wa kaskazini wa Kidal nchini Mali.
Kundi la wanamgambo la Tuareg linaloungwa mkono na Serikali linasemekana kuchukua udhibiti wa mji wa kaskazini wa Kidal nchini Mali, baada ya mapigano kuzuka na kundi lilioundwa na watu waliokuwa waasi wa Tuareg.
Mtu alieshuhudia aliambia VOA idhaa ya Kifaransa kuwa wapiganaji wa Gatia walikuwa wakifanya msako kwenye mji huo Alhamisi jioni ili kuwasaka waasi waliojificha.Hata hivyo hali mjini humo ingali haieleweki na haijabainika kama kuna majeruhi wowote.
Kiongozi wa muungano wa Tuareg Ambeyri Ag Rissa,ameambia maafisa wa VOA kuwa alikuwa akitoka kwenye mkutano kuhusu uuwiano uliotiwa saini Jumapili kuhusu ugavi wa udhibiti kwenye mji huo baada ya mapigano kuzuka. Milio ya risasi ilisikika nyuma yake wakati akizungumza.
Hali mjini humo imebaki kuwa tete hata baada ya mkataba huo kutiwa saini huku pande zote zikilaumiana kwa kuzuka tena kwa mapigano

Popular posts from this blog

MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA SABA 2015 YOTE HAYA HAPA

Angalia yote hapa NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA PSLE-2015 EXAMINATION RESULT ARUSHA DAR ES SALAAM DODOMA IRINGA KAGERA KIGOMA KILIMANJARO LINDI MARA MBEYA MOROGORO MTWARA MWANZA PWANI RUKWA RUVUMA SHINYANGA SINGIDA TABORA TANGA MANYARA GEITA KATAVI NJOMBE SIMIYU   

HUYU NDIE MWANAUME"[SHOGA] MWENYE MAKALIO MAKUBWA KULIKO WOTE DUNIANI,KAAMUA KUPOST HIZI PICHA INSTAGRAM.

Kutana na mwanaume mwenye makalio makubwa kama mwanamke.Kwa jina anaitwa Micah,ni mwanaume ambaye hipsi na makalio yake zinazidi hata zile za wanawake huwezi kuamini hebu tazama hapa utakubali tu mwenyewe.

Fasihi simulizi na Chimbuko la Riwaya

                                                                    Fasihi simulizi na Andishi HISTORIA YA FASIHI SIMULIZI YA KIAFRIKA KWA MTAZAMO WA NADHARI ZA UTANDAWAZI, UTAIFA NA HULUTISHI . Utangulizi Fasihi simulizi kwa mujibu wa Mlokozi (1996), ni fasihi inayotungwa au kubuniwa kichwani na kuwasilishwa kwa hadhira kwa njia ya mdomo na vitendo bila kutumia maandishi. Hivyo fasihi simulizi inafungamana   na muktadha au mazingira fulani ya kijamii na kutawaliwa na muingiliano wa mambo kama vile Fanani, Hadhira, Fani inayotendwa, Tukio, Mahali pamoja na Wakati wa utendaji.             Balisidya (1983) anasema fasihi simulizi ni aina ya fasihi ambayo hutumia mdomo katika kuumbwa, kuwasilishwa na kusambazwa kwa wasikilizaji na watumiaji wake. Mt...